Tuesday, June 18, 2013

K'NJARO UPDATE: KITAYOSCE YAMDUNGUA GOLANI FC KIDUCHU, MKOMBOZI CUP



KITAYOSCE FC TOLEO NA. 006
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
 KITAYOSCE FC



 GOLANI FC





MKOMBOZI CUP imeendelea tena leo kwa Kundi A kuumana vikali katika Uwanja wa Mandela Mjini Moshi Mkoa Kilimanjaro kwa Bingwa Mtetezi wa Kombe hilo kumzaba kwa tabu Golani FC kwabao 1-0.

Mechi hiyo iliyochezeshwa vizuri na Waamuzi Chipukizi kutoka Arusha ilianza majira ya saa 10:40 jioni ya leo kwa timu zote kuwa kamili bila matatizo yoyote.

Kipindi cha Kwanza kilimalizika kwa timu zote kutoliona lango la kila mmojawapo, huku kila timu ikishambuliana kwa zamu.

Dakika ya 78 ya mchezo Kitayosce FC walipata penati iliyopigwa na Jumaa Mgunya baada ya Beki ya Golani FC iliyokuwa ikifanya kazi ya ziada leo Kulwa Hamis alipounawa katika eneo la hatari.

Vikosi vya Leo
Golani FC
Yude Gahambi, Coloman Lucas, Peter Massawe, Hajib Dismas Mpapaio, Kulwa Hamis, Maulid Jumanne, Hamis Yusuf Hamis, Bahati Msele, Jeru Jonathan na Said Ally.

Kitayosce FC
Mussa Juma, Petro Mwaipopo, Annuary Mkondo, Jumaa Mgunya, Stanley Alexander, MeshaCollins, Kibwana Abdallah/ David John, Iddi Shaban/ Julius Ernest, Victor Nduzero, Festo Antony na David Maganga.  

Kwa upande wake Kocha wa Golani FC Swaleh Mhina ameulalamikia mchezo wa leo hasa ukizingatia kulikuwa na mkanganyiko wa maamuzi kati ya mwamuzi wa kati na  mwamuzi wa pembeni ya uwanja.

Swaleh ameahidi kuwa atajitahidi katika michezo ijayo ili aweze kufuzu katika hatua ya Robo Fainali.

Kitayosce FC Inaongoza kundi A ikiwa na Pointi 6 ikiwa imebakiwa na mchezo mmoja katika kundi hilo ambao utachezwa Jumamosi ya Juni 22 mwaka huu dhidi ya Nyuki FC
Mechi za Kesho zitaendelea kama kawaida ambapo Kundi B na C zitavutana mashati.

Kundi B Mvuleni itapambana vikali na Nazareth FC katika uga wa King George Memorial na Kundi C New Generation itavutana na Moshi United katika uga Mandela kata ya Pasua.

Imetolewa na:
JOHNSON JABIR
Msemaji wa Klabu ya Kitayosce
Moshi-Kilimanjaro, Tanzania
+255-(0)-752 319 305

K'NJARO UPDATE: WAZIRI MKUU PINDA MJINI MOSHI LEO



WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA LEO AMEFUNGUA MRADI WA BENKI YA DUNIA KWA HALMASHAURI ZOTE HAPA NCHINI. MKUTANO HUO UMEFANYIKA KATIKA MJI WA MOSHI UKIHUDHURIWA NA WAZIRI HAWA GHASIA (TAMISEMI).


 WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA



 WAJUMBE WA SEMINA HIYO KUTOKA HALMASHAURI MBALIMBALI NCHINI TANZANIA



 HAWA GHASIA, WAZIRI TAMISEMI




 WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA

TANZANIA FOOTBALL NEWS: KLABU THAILAND YASAKA WACHEZAJI TANZANIA



http://soccerblogs.net/images/blogs/833/medium2.jpgKlabu ya Thai Port Football ya Thailand inatafuta wachezaji nchini Tanzania kwa ajili ya kucheza mpira wa miguu nchini humo na katika nchi nyingine barani Ulaya.

Kupitia kwa wakala wake, klabu hiyo imetuma taarifa kupitia Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ikitaka wachezaji wenye umri kuanzia miaka 15 hadi 28 kwa ajili ya kuwafanyia majaribio ambapo watakaofuzu watacheza nchini humo na katika klabu nyingine za Ulaya ambazo wana ushirikiano nazo.

Wachezaji wenye nia ya kufanya majaribio wanatakiwa kutuma taarifa za wasifu wao (CV) kwa klabu hiyo kwa njia ya emaili, wawe na pasi ya kusafiria pamoja na pasi ya mchezaji (player passport).

Wakala atapitia vitu hivyo, na kwa wachezaji atakaowahitaji atawatumia tiketi za ndege na viza kwa ajili ya kwenda kufanya majaribio nchini humo, na watakaofanikiwa kabla ya kusaini nao mikataba watawasiliana na klabu zao nchini (kwa wale wenye klabu).

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

TANZANIA FOOTBALL NEWS: MTANZANIA APEWA ITC ACHEZE YEMEN



http://2.bp.blogspot.com/-PPp2IXpaP5Y/Txk52BJmw9I/AAAAAAAAETQ/DDznTiZJz4Y/s400/tff+LOGO.jpgShirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetoa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) kwa mchezaji Mtanzania Gossage Mtumwa ili aweze kucheza mpira nchini Yemen.

Mtumwa ambaye anatoka katika kituo cha kukuza na kuendeleza vipaji cha Rollingstone cha Arusha aliombewa hati hiyo na Chama cha Mpira wa Miguu cha Yemen (YFA) kwa ajili ya kucheza nchini humo.

TFF inamtakia kila la kheri Mtumwa katika safari yake ya Yemen, na ni matarajio yetu kuwa atakuwa balozi mzuri wa Tanzania nchini humo ili wachezaji wengine wa Tanzania nao wapate fursa ya kucheza mpira wa miguu nchini Yemen.

AFRICA NEWS: RWIZA KUHUDHURIA SEMINA YA MAKAMISHNA CAF



http://upload.wikimedia.org/wikipedia/so/a/a6/Caf-logo-.jpg
Kamishna Alfred Kishongole Rwiza ameteuliwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) kuhudhuria semina ya makamishna itakayofanyika kuanzia Julai 6-7 mwaka huu katika makao makuu ya shirikisho hilo jijini Cairo, Misri.

Semina hiyo inashirikisha baadhi ya makamishna wa CAF walioko kwenye orodha ya makamishna ya shirikisho hilo kwa mwaka 2012-2014.

Rwiza ni mmoja wa makamishna wa CAF kutoka Tanzania, na mechi ya mwisho kusimamia ilikuwa ya Kombe la Shirikisho iliyochezwa Mei mwaka huu nchini  Msumbiji.

CAF tayari imeshamtumia tiketi Rwiza, na anatarajia kuondoka nchini Julai 4 mwaka huu kwenda Cairo kwa ndege ya EgyptAir.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

G


website counters

BLOGU NYINGINE