KITAYOSCE
FC TOLEO NA. 006
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
KITAYOSCE
FC
GOLANI
FC
MKOMBOZI
CUP imeendelea tena leo kwa Kundi A kuumana vikali katika Uwanja wa Mandela
Mjini Moshi Mkoa Kilimanjaro kwa Bingwa Mtetezi wa Kombe hilo kumzaba kwa tabu
Golani FC kwabao 1-0.
Mechi hiyo iliyochezeshwa
vizuri na Waamuzi Chipukizi kutoka Arusha ilianza majira ya saa 10:40 jioni ya
leo kwa timu zote kuwa kamili bila matatizo yoyote.
Kipindi cha Kwanza kilimalizika
kwa timu zote kutoliona lango la kila mmojawapo, huku kila timu ikishambuliana
kwa zamu.
Dakika ya 78 ya mchezo
Kitayosce FC walipata penati iliyopigwa na Jumaa Mgunya baada ya Beki ya Golani
FC iliyokuwa ikifanya kazi ya ziada leo Kulwa Hamis alipounawa katika eneo la
hatari.
Vikosi vya Leo
Golani
FC
Yude Gahambi, Coloman Lucas,
Peter Massawe, Hajib Dismas Mpapaio, Kulwa Hamis, Maulid Jumanne, Hamis Yusuf
Hamis, Bahati Msele, Jeru Jonathan na Said Ally.
Kitayosce
FC
Mussa Juma, Petro Mwaipopo,
Annuary Mkondo, Jumaa Mgunya, Stanley Alexander, MeshaCollins, Kibwana
Abdallah/ David John, Iddi Shaban/ Julius Ernest, Victor Nduzero, Festo Antony
na David Maganga.
Kwa upande wake Kocha wa Golani
FC Swaleh Mhina ameulalamikia mchezo wa leo hasa ukizingatia kulikuwa na
mkanganyiko wa maamuzi kati ya mwamuzi wa kati na mwamuzi wa pembeni ya uwanja.
Swaleh ameahidi kuwa
atajitahidi katika michezo ijayo ili aweze kufuzu katika hatua ya Robo Fainali.
Kitayosce FC Inaongoza kundi A
ikiwa na Pointi 6 ikiwa imebakiwa na mchezo mmoja katika kundi hilo ambao
utachezwa Jumamosi ya Juni 22 mwaka huu dhidi ya Nyuki FC
Mechi za Kesho zitaendelea kama
kawaida ambapo Kundi B na C zitavutana mashati.
Kundi B Mvuleni itapambana
vikali na Nazareth FC katika uga wa King George Memorial na Kundi C New
Generation itavutana na Moshi United katika uga Mandela kata ya Pasua.
Imetolewa
na:
JOHNSON
JABIR
Msemaji
wa Klabu ya Kitayosce
Moshi-Kilimanjaro,
Tanzania
+255-(0)-752
319 305


